• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua za Ofisi |
    • Malalamiko |
Bunda Town Council
Bunda Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vision
    • Miiko ya Halmashauri
    • Mikakati
  • Utawala
    • Chati ya Halmashauri
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
    • Idara Mbali mbali
      • Utumishi na Utawala
      • Idara ya Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Urban Planning and Natural Resources
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Kilimo na Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Miundombinu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na mwenyekiti
    • Kata
      • Kata ya Balili
      • Kata ya Kabasa
      • Kata ya Mcharo
      • Kata ya Manyamanyama
      • Kata ya Sazira
      • Kata ya Wariku
      • Kata ya Nyatwali
      • Kata ya Guta
      • Kata ya Kabarimu
      • Kata ya Bunda Stoo
      • Kata ya Nyasura
      • Kata ya Nyamakokoto
      • Kata ya Kunzugu
      • Kata ya Bunda mjini
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayo endelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Hotuba
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWENGE WA UHURU 2024 WATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO 9

Posted on: August 3rd, 2024

UTANGULIZI

Halmashauri ya Mji wa Bunda ni Miongoni mwa Halmashauri 9 za Mkoa wa Mara. Katika Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024, Halmashauri ya Mji wa Bunda imekimbiza Mwenge leo Jumamos tarehe 03.08.2024 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Uwapo katika Halmashauri ya Mji wa Bunda Mwenge wa Uhuru umekimbizwa umbali wa Kilometa 94 chini ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Godfrey Eliakimu Mnzava. Mwenge wa Uhuru Umezindua, kuweka jiwe la Msingi na kutembelea Miradi 10.

MCHANGANUO WA MIRADI

Matukio mbalimbali yaliyotokea katika miradi ni kama ifuatavyo:

MIRADI ILIYOZINDULIWA

Kituo Jumuishi cha Urasimishaji na Uendelezaji wa Biashara. Mradi unathamani ya shilingi 100,420,815.00. Unapatikana Kata ya Bunda stoo. Maoni ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge amesema mradi ni mzuri na amekubali kuweka jiwe la msingi

Hotel ya Golden Peak (Golden Peak Hotel). Mradi unathamani ya shilingi 209,000,000.00 Hotel hii ni mali ya mtu binafsi. Katika kutambua mchango wa Sekta binafsi, Serikali imeona ni vema mradi huu ukazinduliwa na Mwenge wa Uhuru. Kiongozi wa Mbio za Mwenge amekubali kufungua Mradi.

MIRADI ILIYOWEKEWA JIWE LA MSINGI

Zahanati ya Ligamba. Mradi huu umeenzishwa kwa nguvu za wananchi na baadae kushikwa mkono na Serikali kwa shilingi milioni 50. Jumla ya thamani ya mradi hadi sasa ni shilingi 53,390,800.00 Maoni ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amekubali kuwekanjiwe la msingi na kupongeza juhudi za wananchi kuanzisha ujenzi.

Ujenzi wa Bweni la Watoto wenye mahitaji maalum. Mradi unathamani ya shilingi 160,000,000.00 ikiwa milioni 130 kutoka Serikali Kuu na milioni 30 kutoka Mapato ya ndani ya Halmashauri ya Mji wa Bunda. Maoni ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amekataa kuweka jiwe la msingi kutokana na kuwa na mashaka na gharama za mradi zilizotumika na zinazohitajika kukamilisha mradi.

Ujenzi wa Madarasa sita na matundu nane ya vyoo. Mradi umejengwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu wenye thamani ya shilingi 168,000,000.00. Mradi umegfikia hatu ya ukamilishaji. Maoni ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amekubali kuweka jiwe la msingi kuutaka uongozi kuendelea kusimamia vizuri mradi ukamilike kwa wakati. 

Ujenzi wa Mradi wa kuchakata maji taka Bunda Mjini. Mradi unathamani ya shilingi 1,728,019,700.00. Maoni ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amekubali kuweka jiwe la msingi ujenzi uendelee. 

Ujenzi wa Daraja la Bigutu – Nyasana. Mradi unathamani ya shilingi 232,970,000.00 Mradi upo katika kata ya Bunda stoo. Daraja hili limerahisisha shughuli za kiuchumi ya Wananchi wa Kata ya Kabasa na Bunda stoo. Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amekubali kuweka jiwe la msingi.

MIRADI ILIYOTEMBELEA

Jengo la Radiolojia. Mradi huu ulizinduliwa na Mwenge wa Uhuru Mwaka 2023 hivyo Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa zimeutembelea kutazama uendelevu wa mradi. Mradi upo katika Kituo cha Afya Manyamanyama. Maoni ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amekubali kutembelea mradi

Kikundi cha Vijana Kazi Kazi (Kazi kazi Group). Kikundi kinajihusisha na Uuzaji wa nguo za Mitumba. Kikundi kinamtaji wa Shilingi milioni 2,900,000.00, kati ya hiyo fedha shilingi 2,000,000.00 walipataka kutoka katika mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Mapato ya ndani ya Halmashauri ya Mji wa Bunda. Maoni ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amekubali kutembelea kikundi.

Mradi wa Mazingira katika shule ya sekondari Sazira. Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ulitembelea mradi wa Mazingira katika shule ya sekondari Sazira na kupata taarifa ya Upandaji miti kuanzi Julai 2023 hhadi Julai 2024 ambapo Halmashauri imefanikiwa kupanda miti 395,284.

Lakini pia Mwenge wa Uhuru umepanda miti 50 na kugawa miti 1000 kwa wananchi wa eneo hilo katika shule hiyo. Maoni ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amekubali kutembelea mradi na kkupanda miti.

Mwisho Mwenge wa Uhuru ulielekea katika eneo la Mkesha ambapo ulikagua Kongamano/Mdahalo wa Vijana, Banda ya Ujasiliamali, Uchaguzi na Baadae kusoma Risala ya Utii.

Matangazo Mengine

  • TANGAZO LA KAZI KADA MBALIMBALI September 17, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA UANDIKISHAJI WA WAPIGA KURA SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI KADA YA AFYA September 12, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI AMREF HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA August 31, 2024
  • Soma yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA BUNDA YAKAGUA NA KURIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 1.09 IKIWA NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM

    March 12, 2025
  • RC MARA AMPOKEA DC BUNDA

    February 27, 2025
  • DC BUNDA DKT. VICENT ANNEY ALISHAURI BARAZA LA MADIWANI KUPANGA BAJETI YENYE TIJA KWA MAENDELEO YA HALMASHAURI

    February 13, 2025
  • ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 32.2 ZAPITISHWA NA BARAZA LA MADIWANI IKIWA NI MPANGO NA BAJETI WA 2025/2026

    February 13, 2025
  • Soma yote

Video

Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2017
  • Matokeo ya Kidato cha nne 2017
  • SHERIA YA MANUNUZI
  • Training Guide for updating and Preparation of District Strategic Plans
  • Majukumu ya Viongozi Ngazi ya Halmashauri
  • Land Act 2004
  • HOTUBA YA BAJETI OR - TAMISEMI
  • ORODHA YA WALIMU WAPYA

Kurasa za kufanana

  • Wizara ya Habari
  • Wizara ya Utumishi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • OR TAMISEMI
  • Mkoa wa Mara
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Bunda Town Council

    Anuani ya Posta: 219 Bunda

    Sim: +255 28 2621773

    Mobile:

    Barua Pepe: info@bundatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

haki zote zimehifadhiwa.Haki miliki ©2017 Halmashauri ya mji wa bunda