• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua za Ofisi |
    • Malalamiko |
Bunda Town Council
Bunda Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vision
    • Miiko ya Halmashauri
    • Mikakati
  • Utawala
    • Chati ya Halmashauri
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
    • Idara Mbali mbali
      • Utumishi na Utawala
      • Idara ya Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Urban Planning and Natural Resources
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Kilimo na Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Miundombinu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na mwenyekiti
    • Kata
      • Kata ya Balili
      • Kata ya Kabasa
      • Kata ya Mcharo
      • Kata ya Manyamanyama
      • Kata ya Sazira
      • Kata ya Wariku
      • Kata ya Nyatwali
      • Kata ya Guta
      • Kata ya Kabarimu
      • Kata ya Bunda Stoo
      • Kata ya Nyasura
      • Kata ya Nyamakokoto
      • Kata ya Kunzugu
      • Kata ya Bunda mjini
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayo endelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Hotuba
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ZIARA YA NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS TAMISEMI MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA KUKAGUA UJENZI WA MADARASA

Posted on: December 21st, 2021

“Nimefika hapa Bunda Mji niwapongeze kwa kazi nzuri ambazo mnaendelea nazo za ujenzi wa Madarasa. Madarasa ukiyaona yanaviwango, tofali zimenyoka ziko vizuri unaona kabisa kuna ushirikiano mkubwa wa mafundi katika kazi na nimeambiwa kwamba tofali hizi mnafyatua wenyewe kwenye kiwanda cha Halmashauri jambo ambalo ni ubunifu mzuri wa kuongeza mapato ya Halmashauri. Lazima Halmashauri nyingine zijifunze kupitia Halmashauri hizi.”

Hayo yamesemwa na Mheshimiwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Dkt. Festo J. Dugange wakati akitembelea na kukagua ujenzi wa madarasa 59 unaoendelea ndani ya Halmashauri ya Mji wa Bunda. Mheshimiwa Waziri amesema lengo la ziara hii ni kushirikiana, kushauriana na kupeana mawazo ya namna ya kutekeleza ujenzi wa miradi ya elimu, afya na miradi mingine ambayo ina dhumuni la kuboresha huduma za jamii na kuwezesha wanafunzi wa Sekondari na shule za Msingi katika kujifunza katika mazingira bora.

Mheshimiwa Naibu Waziri ameongeza kwa kusema kuwa miradi hii inatakiwa kukamilika tarehe 30/12/2021 licha ya changamoto za vitendea kazi zilizojitokeza ambazo zilikua ni za nchi nzima. "Jambo la Msingi Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi mjipange kuongeza nguvukazi usiku na mchana kukamilisha ujenzi huu kama mlivyokubaliana kukabidhi kwa RAS tarehe 27/12/2021." Amesisitiza Mheshimiwa Dugange.

Mheshimiwa Naibu Waziri ameeleza kuwa Mheshimiwa Rais ameleta fedha nyingi sana akiwa na imani na watu wanaozisimamia. Amisitiza kuwa Mwezi Januari kutakuwa na chaguo moja tu la wanafunzi na wote watatakiwa kuingia darasani.

Katika ziara hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Ndg. Albert Msovela amemweleza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba jambo la KIPEKEE na la utofauti katika ujenzi uliofanywa na Halmashauri ya Mji wa Bunda ni kwamba wameweka vigae madarasani na kujenga Ofisi za Walimu katikati ya madarasa hayo.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe. Joshua Nassari amemueleza Mheshimiwa Naibu Waziri kuwa kitu ambacho kimechelewesha kasi ya ujenzi huu ni upatikanaji wa saruji, jambo ambalo aliamua kulivalia njuga kwenda Tanga kiwandani na kufanikisha kulipia mifuko ya saruji elfu kumi na saba (17,000) na kusafirisha kutoka Tanga hadi Bunda ili kukabiliana na Changamoto ya Saruji hususani katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda yenye miradi mingi ikiwemo ya Ujenzi wa Vituo vya Afya, Hospitali ya Wilaya, Jengo la huduma za dharura,  Madarasa na ujenzi wa Jengo la Ofisi za Halmashauri. Hata hivyo, Mheshimiwa Nassari amesema kwa sasa ujenzi huu utaenda kasi kwasababu uwepo wa saruji ya kutosha.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Ndg. Emmanuel Mkongo amemuomba Mheshimiwa Naibu Waziri kusaidia kutatua shida ya Maji katika shule ya Sekondari Bunda ambayo ni shule ya bweni wasichana na Wavulana kwa kidato cha tano na sita, ambapo Mheshimiwa Naibu Waziri  amelichukua kwa utekelezaji Zaidi.

Matangazo Mengine

  • TANGAZO LA KAZI KADA MBALIMBALI September 17, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA UANDIKISHAJI WA WAPIGA KURA SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI KADA YA AFYA September 12, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI AMREF HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA August 31, 2024
  • Soma yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA BUNDA YAKAGUA NA KURIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 1.09 IKIWA NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM

    March 12, 2025
  • RC MARA AMPOKEA DC BUNDA

    February 27, 2025
  • DC BUNDA DKT. VICENT ANNEY ALISHAURI BARAZA LA MADIWANI KUPANGA BAJETI YENYE TIJA KWA MAENDELEO YA HALMASHAURI

    February 13, 2025
  • ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 32.2 ZAPITISHWA NA BARAZA LA MADIWANI IKIWA NI MPANGO NA BAJETI WA 2025/2026

    February 13, 2025
  • Soma yote

Video

Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2017
  • Matokeo ya Kidato cha nne 2017
  • SHERIA YA MANUNUZI
  • Training Guide for updating and Preparation of District Strategic Plans
  • Majukumu ya Viongozi Ngazi ya Halmashauri
  • Land Act 2004
  • HOTUBA YA BAJETI OR - TAMISEMI
  • ORODHA YA WALIMU WAPYA

Kurasa za kufanana

  • Wizara ya Habari
  • Wizara ya Utumishi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • OR TAMISEMI
  • Mkoa wa Mara
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Bunda Town Council

    Anuani ya Posta: 219 Bunda

    Sim: +255 28 2621773

    Mobile:

    Barua Pepe: info@bundatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

haki zote zimehifadhiwa.Haki miliki ©2017 Halmashauri ya mji wa bunda