• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua za Ofisi |
    • Malalamiko |
Bunda Town Council
Bunda Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vision
    • Miiko ya Halmashauri
    • Mikakati
  • Utawala
    • Chati ya Halmashauri
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
    • Idara Mbali mbali
      • Utumishi na Utawala
      • Idara ya Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Urban Planning and Natural Resources
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Kilimo na Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Miundombinu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na mwenyekiti
    • Kata
      • Kata ya Balili
      • Kata ya Kabasa
      • Kata ya Mcharo
      • Kata ya Manyamanyama
      • Kata ya Sazira
      • Kata ya Wariku
      • Kata ya Nyatwali
      • Kata ya Guta
      • Kata ya Kabarimu
      • Kata ya Bunda Stoo
      • Kata ya Nyasura
      • Kata ya Nyamakokoto
      • Kata ya Kunzugu
      • Kata ya Bunda mjini
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayo endelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Hotuba
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YALETA TUMAINI JIPYA KWA WATOTO YATIMA BUNDA MJINI.

Posted on: March 7th, 2021

HALMASHAURI ya Mji wa Bunda imeadhimisha siku ya wanawake duniani katika kituo cha watoto yatima cha ST. FRANCIS WA ASSIZ kilichopo kata ya Kunzugu leo tarehe 07/03/2021. Maadhimisho haya yameambatana na kutoa misaada mbalimbali kwa watoto kama unga mchele, sabuni za kufulia, juice, sukari, madaftari, kalamu, mafuta ya kupaka na ya kupikia na vitu vingine vingi.

Mgeni rasmi katika tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Mwalimu Lydia Simion Bupilipili ameipongeza Halmashauriya Mji wa Bunda kwa kuwathamini watoto yatima na wenye mazingira magumu kwa kuchagua kuadhimisha tukio hili katika kituo hiki. Amesema kitendo hiki kitatambulisha kituo kwa watu wengi zaidi maana wengi walikua hawakifahamu. Hivyo amewaomba wananchi wote kujitokeza kwa wingi kuwasaidia watoto hawa kwa chochote wanachobarikiwa.

Aidha mgeni rasmi, amewataka wanawake kujitambua na kujielewa, kuamka na kuchakarika na kujihusisha na shughuli mbalimbali zitakazowaingizia kipato na sio kubweteka, kukaa kusubiri mwanaume awatimizie kila kitu.

Kwa upande wa viongozi, Mheshimiwa mgeni rasmi amewataka viongozi wanawake kuwatumikia wananchi kwa haki na usawa kwa wote ili kuifikia dunia yenye usawa.

Mwenyekitiwa Halmashauri ya Mji wa Bunda ndugu Michael Kweka, ameushukuru uongozi wa kituo cha watoto Yatima kukubali kufanyia maadhimisho ya siku ya wanawake duniani katika kituo hiki. Aidha amewaomba wakazi wa mji wa bunda kuwa mabarozi kwa watu wote kujitoa kwa moyo kukisaidia kituo hiki.

Awali Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Bi. Janet Mayanja alieleza jinsi wananchi walivyoguswa kuwachangia watoto yatima katika maadhimisho haya. Amesema kuwa “makundi mbalimbali yamejitokeza kuleta zawadi kwa watoto akiwemo Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, viongozi mbalimbali wa Vyama, Taasisi na Serikali na vikundi mbalimbali vya kijasiliamali.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda, amewaomba sana wanawake wa Halmashauri ya Mji wa Bunda kuwasomesha watoto wao ili kuwaandaa kuwa viongozi wa baadae. Na pia amewapongeza wanawake ambao wamejiunga na vikundi vya Vicoba na kuwajulisha kwamba sasaivi Wizara ya fedha kwa kushirikiana na benki kuu imeandaa utaratibu wa kuvitambua na kuvirasimisha vikundi vyote vya Vicoba. Hii itasaidia vikundi vingi kukopesheka katika taasisi mbalimbali za kifedha kwa urahisi.

Aidha, Wageni mbalimbali waliakwa kushiriki maadhimisho haya na baadhi yao walitoa salamu kwa wanawake waliojitokeza kwa wingi kusherehekea siku ya wanawake Duniani.

Katibu wa CCM wa Wilaya ya Bunda alitoa neno kwa kusema “Wanawake ni jeshi kubwa na sisi tuliozaliwa na mwanamke tunamthamini sana mwanamke kwamba ndie mkombozi na Kila mwanaume aliefanikiwa basi kuna mwanamke nyuma yake”

Naye mwakilishi kutoka ofisi ya TANAPA kanda ya Magharibi, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Maendeleo ya Utalii Bi. Neema Philipo Mollel, Amewahamasisha wanawake wa Halmashauri ya Mji wa Bunda kufanya utalii katika hifadhi bora kuliko zote Afrika, hifadhi ya Serengeti iliyopo katika mazingira yetu. Amesema “TANAPA imeandaa ofa ya kwenda kutalii kwa makundi kwa kutumia usafiri wa basi kwa gharama nafuu ya shilingi elfu Arobaini inayojumlisha gharama za usafiri wa kwenda na kurudi pamoja na chakula. Ofa hii itaendelea hadi sikukuu ya Pasaka.

Kauli mbiu ya siku ya wanawake duniani kwa mwaka 2021 inasema, : Wanawake katika Uongozi: Chachu kufikia dunia yenye usawa.

Matangazo Mengine

  • TANGAZO LA KAZI KADA MBALIMBALI September 17, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA UANDIKISHAJI WA WAPIGA KURA SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI KADA YA AFYA September 12, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI AMREF HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA August 31, 2024
  • Soma yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA BUNDA YAKAGUA NA KURIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 1.09 IKIWA NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM

    March 12, 2025
  • RC MARA AMPOKEA DC BUNDA

    February 27, 2025
  • DC BUNDA DKT. VICENT ANNEY ALISHAURI BARAZA LA MADIWANI KUPANGA BAJETI YENYE TIJA KWA MAENDELEO YA HALMASHAURI

    February 13, 2025
  • ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 32.2 ZAPITISHWA NA BARAZA LA MADIWANI IKIWA NI MPANGO NA BAJETI WA 2025/2026

    February 13, 2025
  • Soma yote

Video

Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2017
  • Matokeo ya Kidato cha nne 2017
  • SHERIA YA MANUNUZI
  • Training Guide for updating and Preparation of District Strategic Plans
  • Majukumu ya Viongozi Ngazi ya Halmashauri
  • Land Act 2004
  • HOTUBA YA BAJETI OR - TAMISEMI
  • ORODHA YA WALIMU WAPYA

Kurasa za kufanana

  • Wizara ya Habari
  • Wizara ya Utumishi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • OR TAMISEMI
  • Mkoa wa Mara
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Bunda Town Council

    Anuani ya Posta: 219 Bunda

    Sim: +255 28 2621773

    Mobile:

    Barua Pepe: info@bundatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

haki zote zimehifadhiwa.Haki miliki ©2017 Halmashauri ya mji wa bunda