• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua za Ofisi |
    • Malalamiko |
Bunda Town Council
Bunda Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vision
    • Miiko ya Halmashauri
    • Mikakati
  • Utawala
    • Chati ya Halmashauri
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
    • Idara Mbali mbali
      • Utumishi na Utawala
      • Idara ya Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Urban Planning and Natural Resources
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Kilimo na Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Miundombinu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na mwenyekiti
    • Kata
      • Kata ya Balili
      • Kata ya Kabasa
      • Kata ya Mcharo
      • Kata ya Manyamanyama
      • Kata ya Sazira
      • Kata ya Wariku
      • Kata ya Nyatwali
      • Kata ya Guta
      • Kata ya Kabarimu
      • Kata ya Bunda Stoo
      • Kata ya Nyasura
      • Kata ya Nyamakokoto
      • Kata ya Kunzugu
      • Kata ya Bunda mjini
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayo endelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Hotuba
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UZINDUZI WA VYUMBA 48 VYA MADARASA HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA

Posted on: January 15th, 2022

Jumla ya madarasa 48 ya shule za Sekondari 15 za Halmashauri ya Mji wa Bunda yaliyojengwa kupitia Mpango wa Maendeleo ya Ustawi wa Taifa yamepokelewa na kuzinduliwa rasmi leo tarehe 15/01/2022 na Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda Bw. Salumu Mtelela kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Bunda.

Katibu Tawala amemshukuru na kumpongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha za ujenzi wa madarasa hayo ambayo yatachangia kuboresha elimu nchini.

Katibu Tawala ameeleza kuwa licha ya changamoto zilizokuwa zikijitokeza wakati wa utekelezaji wa mradi lakini Uongozi ulipambana kuhakikisha kazi inaendelea. Aidha,  amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Ndugu Emmanuel J. Mkongo kwa ubunifu na kujiongeza kupitia mradi huu kujenga Ofisi 30 zenye uwezo wa kubeba walimu 8 katika shule zote za Sekondari zilizotekeleza mradi huu.

Mheshimiwa mgeni rasmi hakusita kutoa wito kwa walimu kuhakikisha wanayatunza madarasa hayo ili kuhakikisha yanadumu katika ubora wake. Pia amepongeza ubunifu wa Ofisi ya Mkurugenzi kuzalisha tofali zenye ubora kutoka katika kiwanda cha Halmashauri ya Mji wa Bunda  ambazo zilitumika kujenga madarasa yote hamsini na tisa (59) yaliyojengwa kupitia mradi huu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bunda, Mhe. Michael Kweka, amesema ushirikiano mzuri baina ya Mkurugenzi, Wataalam, Wakuu wa Shule, Walimu Wakuu, Kamati za Ujenzi, Mafundi na Waheshimiwa Madiwani ndio silaha kubwa iliyowezesha kukamilisha ujenzi huu kwa kiwango kinachostahili.

Aidha, Mwenyekiti amezipongeza Kamati za Ujenzi za Shule chini ya Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu kwa kusimamia vyema mradi huu.

Wakati huo huo Mheshimiwa Mwenyekiti ametoa pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuleta maendeleo nchini hasa kwa kuleta fedha za ujenzi wa madarasa hayo.

Kwaniaba ya Waheshimiwa Madiwani wote Halmashauri ya Mji wa Bunda, Diwani wa Kata ya Kabarimu Mheshimiwa Mhona Nyahimbu ametoa pongezi kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wilaya, Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda na Kamati zake za ujenzi kwa kufanikisha ujenzi wa madarasa hayo katika Kata zote 14 za Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Ndg. Emmanuel Mkongo ameeleza kwamba Halmashauri ilipokea kiasi cha shilingi bilioni 1.18 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa hamsini na tisa (59) kwa shule 15 za Sekondari na shule za Msingi Shikizi tatu. Mkurugenzi ameeleza kuwa hadi leo tarehe 15/01/2022 jumla ya madarasa 48 yamekamilika kwa asilimia 100 na madarasa 11 yaliyosalia yapo katika hatua za ukamilishaji ambapo yatakamilika ndani ya siku 7 zijazo. Aidha kupitia mradi huu Halmshauri imefanikiwa kujenga Ofisi 30 kwa shule zote zilizotekeleza mradi huu, kuweka vigae vyenye ubora kwa kila darasa pamoja na viti na meza 50 kwa kila darasa kwa shule za Sekondari.

Mkurugenzi ameeleza zaidi kuwa mradi huu umechangia kutoa ajira 748 kwa wananchi mbalimbali wakiwemo mafundi. Mkurugenzi ameongeza kwa kusema kuwa mradi huu utasaidia kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza wote kwa mkupuo mmoja.

Matangazo Mengine

  • TANGAZO LA KAZI KADA MBALIMBALI September 17, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA UANDIKISHAJI WA WAPIGA KURA SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI KADA YA AFYA September 12, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI AMREF HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA August 31, 2024
  • Soma yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA BUNDA YAKAGUA NA KURIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 1.09 IKIWA NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM

    March 12, 2025
  • RC MARA AMPOKEA DC BUNDA

    February 27, 2025
  • DC BUNDA DKT. VICENT ANNEY ALISHAURI BARAZA LA MADIWANI KUPANGA BAJETI YENYE TIJA KWA MAENDELEO YA HALMASHAURI

    February 13, 2025
  • ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 32.2 ZAPITISHWA NA BARAZA LA MADIWANI IKIWA NI MPANGO NA BAJETI WA 2025/2026

    February 13, 2025
  • Soma yote

Video

Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2017
  • Matokeo ya Kidato cha nne 2017
  • SHERIA YA MANUNUZI
  • Training Guide for updating and Preparation of District Strategic Plans
  • Majukumu ya Viongozi Ngazi ya Halmashauri
  • Land Act 2004
  • HOTUBA YA BAJETI OR - TAMISEMI
  • ORODHA YA WALIMU WAPYA

Kurasa za kufanana

  • Wizara ya Habari
  • Wizara ya Utumishi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • OR TAMISEMI
  • Mkoa wa Mara
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Bunda Town Council

    Anuani ya Posta: 219 Bunda

    Sim: +255 28 2621773

    Mobile:

    Barua Pepe: info@bundatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

haki zote zimehifadhiwa.Haki miliki ©2017 Halmashauri ya mji wa bunda