• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua za Ofisi |
    • Malalamiko |
Bunda Town Council
Bunda Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vision
    • Miiko ya Halmashauri
    • Mikakati
  • Utawala
    • Chati ya Halmashauri
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
    • Idara Mbali mbali
      • Utumishi na Utawala
      • Idara ya Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Urban Planning and Natural Resources
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Kilimo na Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Miundombinu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kuonana na mwenyekiti
    • Kata
      • Kata ya Balili
      • Kata ya Kabasa
      • Kata ya Mcharo
      • Kata ya Manyamanyama
      • Kata ya Sazira
      • Kata ya Wariku
      • Kata ya Nyatwali
      • Kata ya Guta
      • Kata ya Kabarimu
      • Kata ya Bunda Stoo
      • Kata ya Nyasura
      • Kata ya Nyamakokoto
      • Kata ya Kunzugu
      • Kata ya Bunda mjini
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayo endelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Hotuba
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Uzinduzi wa Upigaji Chapa ya Ng'ombe Halmashauri ya Mji wa Bunda

Sunday 18th, May 2025
@BUTAKALE KATA YA BUNDA STOO

HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA

UZINDUZI WA ZOEZI LA UPIGAJI CHAPA MIFUGO (NG’OMBE)

 

Halmashauri ya Mji wa Bunda, imezindua zoezi la upigaji chapa mifugo (ng’ombe) katika Kata ya Bunda Stoo, mtaa wa Butakare na Migungani tarehe 07/09/2017, uzinduzi ambao ulifanywa na Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh. Lyidia Bupilipili.

Mkuu wa Wilaya aliwapongeza wafugaji na wananchi wote waliojitokeza kwa ajili ya kushuhudia uzinduzi huo na wale ambao walileta ng’ombe kwa ajili ya kupigwa chapa.

Mkuu wa Wilaya aliwaasa kutopuuzia zoezi hilo kwa kuwa ni agizo la Serikali, hivyo ni lazima kila mfugaji ahakikishe ng’ombe wake wote wamepigwa chapa na si vinginevyo, alisisitiza kwamba kwa zoezi la upigaji chapa wafugaji watapumzika na adha za wizi wa mifugo kwa sababu ng’ombe watakuwa wanatambulika kila watakapopita kuwa ni ng’ombe wa eneo fulani.

Pamoja na uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya aliwataka wafugaji wote wa Halmashauri ya Mji wa Bunda kutobweteka na kumiliki makundi makubwa ya mifugo wakati sifa za mji haziruhusu kutenga maeneo ya malisho, kinachotakiwa ni kuvuna mifugo yao mara kwa mara na kufanya shughuli zingine za maendeleo ikiwa ni pamoja na kujenga shule za sekondari kwa ajili ya watoto wao, aliwakumbusha kuwa Kata yao haina shule ya sekondari, hivyo badala ya kutafuta eneo la malisho ya mifugo yao, wahakikishe eneo la kujenga shule linapatikana, baada ya hapo wavune mifugo hiyo na kujenga shule na sio kuwatembeza watoto wao na fimbo tu bila kuwaendeleza kielimu.

Akiongea kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Bi Janeth Peter Mayanja, pamoja na juhudi za wafugaji za kuungana na Serikali kuhakikisha kwamba zoezi hilo linafanikiwa baada ya wataalam wa mifugo kuwaelimisha, aliwaambia faida zingine za upigaji chapa ni pamoja na kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji, udhibiti wa magonjwa ya mifugo na kuimarisha biashara ya mifugo ndani na nje ya nchi, pia Serikali itakuwa na nafasi ya kukaa na kuongea na wafugaji katika kupanga mipango ya uendelezaji mifugo kwa kuwa mifugo yao itakuwa imesajiliwa na kutambuliwa tayari kwa ajili ya kuhudumiwa.

Awali katika taarifa yake kabla ya uzinduzi wa zoezi hilo, Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Bwn Rick Stevens Kaduri alisema, Halmashauri ina lengo la kupiga chapa ng’ombe 77,394 katika Kata zote 14 ambapo kutakuwa na vituo 36, gharama zinazotarajiwa kutumika ni Tsh. 11,850,000.00 (milioni kumi na moja na laki nane na hamsini tu), fedha hizo ni pamoja na gharama za uhamasishaji (mikutano na matangazo), kutengeneza chapa pamoja na nguvu za wananchi.

Matangazo Mengine

  • TANGAZO LA KAZI KADA MBALIMBALI September 17, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA UANDIKISHAJI WA WAPIGA KURA SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI KADA YA AFYA September 12, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI AMREF HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA August 31, 2024
  • Soma yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA BUNDA YAKAGUA NA KURIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA HALMASHAURI YA MJI WA BUNDA YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 1.09 IKIWA NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM

    March 12, 2025
  • RC MARA AMPOKEA DC BUNDA

    February 27, 2025
  • DC BUNDA DKT. VICENT ANNEY ALISHAURI BARAZA LA MADIWANI KUPANGA BAJETI YENYE TIJA KWA MAENDELEO YA HALMASHAURI

    February 13, 2025
  • ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 32.2 ZAPITISHWA NA BARAZA LA MADIWANI IKIWA NI MPANGO NA BAJETI WA 2025/2026

    February 13, 2025
  • Soma yote

Video

Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2017
  • Matokeo ya Kidato cha nne 2017
  • SHERIA YA MANUNUZI
  • Training Guide for updating and Preparation of District Strategic Plans
  • Majukumu ya Viongozi Ngazi ya Halmashauri
  • Land Act 2004
  • HOTUBA YA BAJETI OR - TAMISEMI
  • ORODHA YA WALIMU WAPYA

Kurasa za kufanana

  • Wizara ya Habari
  • Wizara ya Utumishi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • OR TAMISEMI
  • Mkoa wa Mara
  • Ikulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Bunda Town Council

    Anuani ya Posta: 219 Bunda

    Sim: +255 28 2621773

    Mobile:

    Barua Pepe: info@bundatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

haki zote zimehifadhiwa.Haki miliki ©2017 Halmashauri ya mji wa bunda